Baba Mtakatifu Francis asema Mashahidi wa Ufufuko wa Yesu Walikuwa Wanawake

Baba Mtakatifu Francisko, katika Katekesi yake ya Jumatano 3 Aprili alisema kwamba, Ufufuko wa Kristo ni kiini cha imani ya Kanisa, msingi wa matumaini ya utekelezaji wa ahadi za Mungu pamoja na ushindi dhidi ya dhambi na mauti. Akifanunua kanuni ya Imani katika mafundisho yake ya kila Jumatano, Baba Mtakatifu alisema, Mashahidi wa kwanza wa ufufuko wa Kristo walikuwa ni wanawake; waliosukumwa na upendo kwa Kristo kiasi kwamba, wakajihimu kwenda kaburini, huko wakapewa Habari Njema ya Ufufuko waliyowashirikisha Mitume. 
Baba Mtakatifu Francis akihutubia mahojaji katika viwanja vya Mt Petro, Roma

Baba Mtakatifu anasema, hii ni changamoto kwa waamini kuweza kushirikisha ile furaha inayopata chimbuko lake kutoka kwa Kristo Mfufuka. Katika historia ya maisha na utume wa Kanisa, wanawake wamekuwa wepesi kuwafungulia wengine mlango wa imani kwa Kristo, kwani imani ni jibu makini la upendo. 
Maelfu ya watu walifurika kumsikiliza Baba Mtakatifu


Kwa njia ya jicho la imani, waamini pia wanayo bahati ya kukutana na Yesu Kristo Mfufuka na kuonja uwapo wake: katika Maandiko Matakatifu, Ekaristi Takatifu na Sakramenti mbali mbali za Kanisa; matendo ya huruma, wema na msamaha ni matukio ambayo yanaonesha uwapo endelevu wa Kristo katika hija ya maisha ya wafuasi wake hapa duniani. 
Umati ukifuatilia mafundisho ya katekesi ya Papa kila Jumatano


Baba Mtakatifu Francisko anahitimisha Katekesi yake kwa kuwataka waamini, mahujaji na watu wenye mapenzi mema kuimarisha imani yao kwa Kristo Mfufuka ili waweze kuwa kweli ni alama wazi ya ukuu wa maisha na matumaini dhidi ya ubaya, dhambi na kifo.


Baba Mtakatifu akisalimiana na umati uliofika katika Viwanja vya Vatican
Wakubwa kwa wadogo walifurika kumsalimia Baba Mtakatifu


Source: www.radiovaticana.va

Commentaires

Posts les plus consultés de ce blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2023 Wilaya ya Rombo

WHAT DAR ES SALAAM BUS RAPID TRANSIT WILL LOOK LIKE!