Articles

Affichage des articles associés au libellé kifo

TANZIA: PADRE MICHAEL MASSAWE CSSp

Image
Jumuiya ya Wamisionari na Watawa wa Shirika la Roho Mtakatifu wanasikitika kutangaza kifo cha mwanashirika mwenzao Padre Michael Massawe CSSp kilichotokea jumatatu tarehe 26 Octoba 2015 katika mji wa La Croix Valmer nchini Ufaransa. Maziko Maziko yatafanyika Ufaransa Ijumaa Novemba 6 saa nane na nusu mchana (saa za Paris sawa na saa kumi na nusu saa za Afrika Mashariki). Kwa desturi za wamisionari wa Roho Mtakatifu maziko hufanyika mahali alipofia. Historia fupi Padre Michael Massawe alizaliwa Septemba 29 mwaka 1960 katika kijiji cha Keni wilayani Rombo (Kilimanjaro). Aliweka nadhiri za kitawa Julai 6, 1988 katika novisia ya Magamba, Lushoto (Tanga). Alipewa daraja la Upadre tarehe 28 mwezi mei 1993 Usa River mjini Arusha.

TANZIA: MAMA EMMY SHIRIMA AFARIKI DUNIA MJINI PARIS

Image
Tunasikitika kutangaza kifo cha Mama Emmy S. Shirima kilichotokea Mei mosi mjini Paris katika Hospitali ya Hôpital Européen Georges Pompidou mjini Paris.  Mama Shirima alikuwa mfanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania mjini Paris tangu mwaka 2006. Mama Shirima alikuwa mgonjwa tangu mwanzoni mwa mwaka huu. Mwili wa marehemu utasafirishwa kwa ndege kwenda Dar es Salaam, Tanzania Alhamisi Mei 7. Baada ya mwili kufika Dar es Salaam siku ya Ijumaa, ibada ya mazishi itafanyika katika Kanisa Katoliki Parokia ya Bikira Maria Mama wa Mkombozi Sinza Jumamosi Mei 9 saa 7 machana. Baadhi ya waombolezaji wakiwa nje ya Hospitali 'Hôpital Européen Georges Pompidou', Paris Ubalozi wa Tanzania mjini Paris ukishirikiana na Watanzania waishio Ufaransa walifanya ibada ya kuuaga mwili wa Mama Shirima leo jioni katika Hospitali ya Georges Pompidou, Paris. Ibada hiyo ilihudhuriwa na Balozi wa Tanzania, wafanyakazi wa ubalozi wa Tanzania, na wawakilishi kutoka  balozi za Kenya, Uganda, Namib...